kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Monday, January 21, 2013

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA ST.JOHN - DODOMA, AKUTWA AMEFARIKI USIKU WA KUAMKIA LEO

Mwanachuo wa Chuo Kikuu cha St. John  kilichopo  Dodoma amekutwa amefariki maeneo ya kikuyu  usiku wa kuamkia leo.
Mwanafunzi huyo (mwanamke) anayekadiliwa kuwa na umri kati ya miaka 50-52  ambaye pia  inasemekana alikuwa anasoma shahada ya kwanza  ya unesi( Bachelor Degree  in Nursing) mwaka wa tatu, Jana mnamo mishale ya  saa  3 usiku wakati akitoka kujisomea na wenzake (kwenye discussion) alipokuwa akirejea nyumbani kwake (eneo lililopo karibu na chuo hicho) alikutana na watu wanaosemekana kuwa ni vibaka, ambao walimdhuru  na kupelekea kifo chake. Hata hivyo  Dodoma universities  Corner inafatilia kwa ukaribu sana ili kubaini   hasa chanzo kilichopelekea  kifo  cha Mwanachuo huyo.
Ingawa chanzo chetu cha habari kimebaini kuwa mwili wa marehemu (Mwanachuo huyo) ulikutwa mapema Alfajiri ya leo katika maeneo ya chuo hicho, ambapo mbali na kufariki dunia  baadhi ya viungo vya mwili wake vilionekana  kuharibiwa vibaya na wanyama wanaodhaniwa kuwa ni fisi.
Tayari  taratibu zaidi  zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na  kuondolewa kwa mwili huo na kupisha uchunguzi wa  wa jeshi la polisi juu ya chanzo  kilichopelekea kifo cha mwanafunzi huyo.
     
Dodoma universities Corner  itaendelea kuwaletetea habari kamili juu ya kifo cha mwanafunzi huyo....

No comments :

Post a Comment