kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Wednesday, January 2, 2013

MWANAFUNZI WA CBE (DODOMA) APATA AJALI,ANUSURIKA KIFO,NI WAKATI AKIENDESHA GARI SINZA ,DAR ES SALAAM.

 Reward  Massawe

Mwanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Biashara CBE Kampasi ya Dodoma  Bw. Reward Massawe  Juzi Tarehe 31/12/2012 saa saba (7) mchana alinusurika  kifo masaa machache kabla ya kuuona Mwaka 2013.
Ajali hiyo ilitokea jijini Dar es salaam Eneo la sinza  superstar wakati Bw. Reward  akiendesha gari aina ya NADIA yenye usajili  wa nambari  T712 ACR.
Hata hivyo  Dodoma universities Corner ilizungumza na  Bw. Reward  na kutaka kufahamu hasa mazingira ya Ajali hiyo  yalikuwaje,Ambapo Reward alisema"Akiwa eneo hilo la sinza  superstar (kwenye Mataa)  baada ya   kuruhusiwa na taa za barabarani Mara ghafla  alitokea dereva mmoja wa pikipiki (bodaboda) akiwa amempakia abiria  wake  na kulazimisha kuchomekea pikipiki yake  kwa mbele ya gari hilo  kimakosa , hali iliyopelekea  Dereva wa pikipiki (Timotheo Martin) kugongwa na kufariki dunia papohapo huku  abiria wa pikipiki akiwa ameumizwa vibaya  sana"
Kufuatia tukio hilo  Tayari taratibu za ki-usalama zilichukua mkondo wake kwa lengo la kufanya uchunguzi na mazingira ya kutokea kwa ajali hiyo.Ingawa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa kosa lilikuwa ni la Marehemu Timotheo  ambaye alichomekea pikipki yake mbele ya gari alilokuwa akiendesha Bw. Reward.

 "Hakika nimeamini na ntazidi  kuamini Siku zote kwamba  Ajali haina kinga,Sikukutegemea kama hali hii ingetokea.Naamini halikuwa kusudio langu  kwa hali  hii kutokea,  kwani hata mimi  nimenusurika  katika ajali hii.Hiki ni kipindi kigumu kwangu  nahitaji maombi yenu . Maana sio jambo jepesi hata kidogo unaposhuhudia mwenzako akifariki dunia  hata kama  hukukusudia hali hiyo itokee.Kwa sasa   Polisi wanaendelea na kazi yao nadhani hatima ya suala hili itafahamika" Aisema Bw. Reward.
 

No comments :

Post a Comment