kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Sunday, January 6, 2013

KUFUATIA UFISADI WA MILLIONI 15.6 , ULIOFANYWA NA ALIYE KUWA RAISI WA KITIVO CHA S.S.H (UDOM),MARAIS WA VYUO VINGINE SASA MATUMBO JOTO...

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg7fzkqbk0-MBOx-RoMgvwJXb4DLZhDQ1-BgFrpbDv5IpKVr86q6QbBMtKOoJormanvkq6CWPSYj-TgFBPktzbfk_Z5otIKGSGwRSeL4QVz-9rdGRo3U1FvxWdSp6vJTUhTBcn1t2IMwEEK/s200/1.jpg
ALIYEKUWA RAISI WA  KITIVO CHA  SAYANSI YA  JAMII ,SANAA NA LUGHA (UDOM) BW.   IDD MOHAMED
Siku chache baada ya  Aliyekuwa Rais wa  Kitivo cha Sanaa ya Jamii, Sanaa na  Lugha  (UDOM)  Kutuhumiwa kwa kufanya  ubadhilifu wa  kiasi cha Milioni  15.6 mali ya  Wanafunzi wa chuo  hicho.
Hali hiyo imegeuka fundisho kwa vyuo mbalimbali  hapa nchini. Akizungumza kwa  Masharti ya kutotaja jina  lake Mwanafunzi mmoja wa chuo cha  St .John  amesema  mara nyingi  viongozi wengi wa serikali za wanafunzi wamekuwa wakijikita  katika hali ya kuzitumia fedha za wanafunzi kinyume na taratibu  na  kutumia fedha kwa lengo la kujinufaisha wenyewe.
Katika hatua nyingine kitendo  hicho pia kimepelekea Viongozi mbalimbali wa serikali za wanafunzi kujitathmini na kupitia upya hesabu zao hili kuepuka kukumbwa na  kashfa za ubadhilifu wa fedha.
Kwa upande mwingine  kitendo cha Rais wa  Kitivo cha Sayansi ya Jamii ,Sanaa na Lugha Bw. Idd  kutiwa nguvuni kimeibua  hisia kali kwa wanavyuo walio wengi  na wengi wao  kuanza kuwa na mawazo ya kuhoji mapato na matumizi ya  Fedha zao kwa mujibu wa katiba za vyuo mbalimbali.
  
 
 


No comments :

Post a Comment