kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Wednesday, January 9, 2013

HAYA YOTE YAMESABABISHWA NA UDOM...


  Bonajesuit  Rischard

Katika Maisha yake Bonajesuit  Rischard   atayakumbuka mengi lakini zaidi  ni kuhusu  safari yake  ndefu ya kimasomo akiwa katika Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) Kitivo cha Sayansi  ya Jamii, Sanaa na  Lugha
 " Mwaka 2012  ni mwaka  ambao watu mbalimbali waliweza kutimiza ndoto zao,lakini kwa  upande wake   anafurahi kuweza kuhitimu elimu yake katika ngazi ya Shahada (Shahada ya kwanza) ya biashara na uhasibu.
Waswahili   wanamsemo flani  wanasema   "kazi sio kufanya kazi  bali kazi ni  kutafuta kazi/kupata kazi" kauli hii inakuwa na maana kubwa  hasa katika kizazi hiki cha sasa ambapo ongezeko la wasomi ni kubwa sana ukilinganisha na fursa za ajira zilizopo.
Sasa anayomatumaini  mapya baada ya  kufanikiwa  kupata  kazi, Anasema  " Vijana wengi tunapenda kujiajiri lakini  kimsingi tunakwamishwa  na  ukosefu wa mitaji  licha ya kuwa na uelewa  wa taaluma mbalimbali za kibiashara (ujasiriamali) ,hivyo inatulazimu kutafuta mahali pa kufanya kazi  ili  mwisho wa siku  tuweze kupata kianzio cha mtaji. Ingawa bado ajira nazo ni changamoto kubwa, Hivyo na mshukuru Mungu kupata  mahali pa kufanya kazi kwa sasa" Alisema  Bonajesuit.
Hata hivyo ,anaongeza kwa kusema  Taaluma aliyoipata UDOM ndiyo  ilimuwezesha yeye kupata ajira aliyo nayo sasa licha ya ushindani mkubwa aliokuwa nao dhidi ya wenzake wakati wa usahili,Hivyo anadiriki kusema  "Hatua ya yeye kupata  Kazi ni kwa Msaada mkubwa wa Chuo Kikuu Cha Dodoma"
 


     

Bonajesuit (wa pili kutoka kulia ) akiwa na wahitimu wenzake katika mahafali  ya tatu ya Chuo kikuu cha Dodoma  (UDOM), Kitivo cha Sayansi  ya Jamii, Sanaa na  Lugha 
 

No comments :

Post a Comment