kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Saturday, January 26, 2013

CBE WANENA "NA SISI TUNAHITAJI ULINZI" ...

                      Baadhi ya  Wanafunzi wa CBE -Dodoma ( Picha na Maktaba yetu)

Wanafunzi wa CBE  wameibuka na kusema  kwamba  wao pia wanaliomba jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi katika maeneo ya Chuo hicho. Akizungumza na Dodoma Universities Corner Mwanafunzi mmoja wa Chuo hicho aiyejitambulisha kwa jina mmoja la  Mackson, Amesema wakati umefika kwa Jeshi la polisi kuimarisha  ulinzi kwa vyuo vyote ikiwemo chuo hicho (CBE). "Wanafunzi wa chuo chetu kwa ujumla wake  wanakadiliwa kufikia  5000 hii ni idadi kubwa , Hostel za chuo chetu hazitoshelezi  kwa idadi hiyo ,hivyo wanafunzi tunalazimika kupanga maeneo yaliyoko  nje ya chuo. Mfano wanafunzi wengi wamepanga maeneo ya Airport, Railway , Makole ,Area A,Area D ,Area E, Ipagala, Chadulu,Mlezi,Kikuyu na wengine wamepanga maeneo ya Nkuhungu. Sasa fikilia sasa hivi tunaelekea kwenye mitihani ya Semester ya kwanza kwa wanafunzi wa Diploma II na Bachelor Degree, kufuatia hali hii wanafunzi wengi huwa tunajisomea hapa chuoni kupitia Discussion   mpaka  mida ya saa tano /saa sita , Kwa hali hii  ulinzi unahitajika kwani  wakati mwingine baadhi ya wanafunzi tunahofia vitisho wakati wa kurudi  katika makazi yetu,  ndio maana naona umuhimu wa jeshi la polisi kuimarisha ulinzi" Alisema Mwanafunzi huyo.
Tusisubiri  mpaka  matatizo yatokee ndio tuamue kuchukua hatua ,Hatua zinatakiwa kuchukuliwa kuanzia sasa..Alisema Bw.Mackson
Hali hii ya wanafunzi kujawa na hofu inakuja ikiwa ni siku chache tangu kuaawa kwa mwanafunzi mmoja wa chuo kikuu cha St.John mkoani Dodoma  na kufuatiwa vitendo vya uvamizi kwa wanafunzi  kwa kuporwa Laptop  na simu zao.Licha ya matukio kama haya kutokea pia kwa wanafunzi wa chuo cha  Usimamizi wa Fedha (IFM) wiki chache zilizopita.

No comments :

Post a Comment