kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Monday, January 28, 2013

TASWIRA YA "MBONI SHOW " ILIYOHUSISHA WANAVYUO WA DODOMA

    Wanachuo wa CBE wakielekea Dodoma Hotel  kushiriki  katika kipindi cha   Mboni Show.


Timu ya  Mboni Show jana ilikuwa mkoani Dodoma  katika Hotel ya Dodoma (Dodoma Hotel) kwa kuwakutanisha  Baadhi ya Wanavyuo kutoka vyuo mbalimbali vya Hapa Dodoma. Hata hivyo mada kubwa iliyojadiliwa  ilikuwa ni kuhusu  MA-  SUGAR DADIES  DHIDI YA VIJANA WA KIKE " Mada hiyo ilitoa fursa kwa wanavyuo hao kuchangia kwa kina sababu ambazo hupelekea  akina dada  hususani  wale wenye umri mdogo  na wale wa vyuoni kushiriki katika vitendo vya ngono.  



        Muonekano wa  Baadhi ya wanachuo mara baad ya Kuwasili Dodoma Hotel

  Jamani Tumetokelezeaaa....
                           
                               Mada ilikuwa safi ....


Wakisikiliza kwa makini kile kilichouwa kinaendelea...



                            Sasa mambo ya meanza....



                        Majadiliano yakiendelea ....

Saturday, January 26, 2013

CBE WANENA "NA SISI TUNAHITAJI ULINZI" ...

                      Baadhi ya  Wanafunzi wa CBE -Dodoma ( Picha na Maktaba yetu)

Wanafunzi wa CBE  wameibuka na kusema  kwamba  wao pia wanaliomba jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi katika maeneo ya Chuo hicho. Akizungumza na Dodoma Universities Corner Mwanafunzi mmoja wa Chuo hicho aiyejitambulisha kwa jina mmoja la  Mackson, Amesema wakati umefika kwa Jeshi la polisi kuimarisha  ulinzi kwa vyuo vyote ikiwemo chuo hicho (CBE). "Wanafunzi wa chuo chetu kwa ujumla wake  wanakadiliwa kufikia  5000 hii ni idadi kubwa , Hostel za chuo chetu hazitoshelezi  kwa idadi hiyo ,hivyo wanafunzi tunalazimika kupanga maeneo yaliyoko  nje ya chuo. Mfano wanafunzi wengi wamepanga maeneo ya Airport, Railway , Makole ,Area A,Area D ,Area E, Ipagala, Chadulu,Mlezi,Kikuyu na wengine wamepanga maeneo ya Nkuhungu. Sasa fikilia sasa hivi tunaelekea kwenye mitihani ya Semester ya kwanza kwa wanafunzi wa Diploma II na Bachelor Degree, kufuatia hali hii wanafunzi wengi huwa tunajisomea hapa chuoni kupitia Discussion   mpaka  mida ya saa tano /saa sita , Kwa hali hii  ulinzi unahitajika kwani  wakati mwingine baadhi ya wanafunzi tunahofia vitisho wakati wa kurudi  katika makazi yetu,  ndio maana naona umuhimu wa jeshi la polisi kuimarisha ulinzi" Alisema Mwanafunzi huyo.
Tusisubiri  mpaka  matatizo yatokee ndio tuamue kuchukua hatua ,Hatua zinatakiwa kuchukuliwa kuanzia sasa..Alisema Bw.Mackson
Hali hii ya wanafunzi kujawa na hofu inakuja ikiwa ni siku chache tangu kuaawa kwa mwanafunzi mmoja wa chuo kikuu cha St.John mkoani Dodoma  na kufuatiwa vitendo vya uvamizi kwa wanafunzi  kwa kuporwa Laptop  na simu zao.Licha ya matukio kama haya kutokea pia kwa wanafunzi wa chuo cha  Usimamizi wa Fedha (IFM) wiki chache zilizopita.

WANAFUNZI UDOM WAPANGA KUFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII VILIVYOPO MKOANI MOROGORO MWEZI WA TATU


  Wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) wamepanga kufanya ziara ya kihistoria mkoani Morogoro mwezi wa tatu. Ziara hiyo ya siku tatu waliyoipa jina la Dom mpaka Moro (bata kwenda bata kurudi) inatarajiwa kufanyika sehemu mbalilmbali za mkoa wa Morogoro. Akizungumza na Mhariri wa Lukaza Blog kwa Njia ya Simu Mratibu wa ziara hiyo Mr AMANI KIZUGUTO ameuambia Mtandao huu  ya kwamba taratibu za awali za maandalizi kwa upande mmoja zimekamilika kwani tayari wameshazungumza na mshauri wa wanafunzi (dean of students) katika maandalizi ya awali. Alisema wanatarajia katika ziara hiyo kutembelea mbuga ya wanyama mikumi,maporomoko ya maji katika milima ya udizungwa huku mazungumzo ya kupitia katika vyuo vikuu mbalimbali vilivyopo Mkoani Morogoro yakiendelea ili kwenda kufanya nao matukio mbalimbali ya kijamii.

Pamoja na kujadili mambo ya kielimu. haya sasa kazi kwenu wana udom kwa wale mtakaopenda kwenda wasilianeni na mratibu kwa simu namba
0717 376735
0769 081122

Friday, January 25, 2013

"A" TO " Z" YA MAANDAMANO YALIYOFANYWA JANA NA WANAFUNZI WA ST JOHN MKOANI DODOMA


Baada ya kutembea mji mzima na mabango yao na kuhakikisha kiu yao imekwisha basi waliamua kurudi chuoni

Wanafunzi baada ya kusubili kwa muda mrefu kibari icho wakaamua kuandaa mabango kwa ajili ya maandamano, ambapo kibari kipatikane kisipatikane walidai kuandamana ni lazima





Mabango yalipokamilika wakasimama kwenye bendera kwa mara nyingine








Walifika mbali na kuona kuwa polisi wanahusika katika mambo mabaya wanayofanyiwa. Ndipo wakachora bango hili kuonyesha hisia zao
Hapa wapo barabarani na masomo kwa siku ya leo hayakuwepo


Bango lina picha ya mwanafunzi alieuliwa kikatili, aliefahamika kwa jina la  Bi.LYDIA





Ni mchaka mchaka ulioendana na nyimbo za hisia



Haya huyu anaashiria demokrasia na maendelea ndio imetawala juu yao

Msafara hapa unaelekea maeneo ya Bungeni

Kila walipopita walikuwa wakishindikizwa na polisi kuhakikisha amani inatawala

Hakuna kitu ambacho kiliniacha hoi baada ya wanafunzi kwenda mpaka Bungeni, kisha walipofika wakaimba nyimbo ya Taifa. Polisi waliwaomba kuongea na viongozi wa maandamano hayo wakajibiwa na wanafunzi kuwa kiongozi wao hameishakufa ambae ni mama LYDIA LEO

Gari la maji ya kuwasha lilikuwepo lakini wanafunzi hao hawakutishika na kitu chochote kile kutoka kwa Polisi



Wanafunzi walifika mpaka Nyerere Square waliimba nyimbo mbalimbali mahala hapo





Baada ya kutembea mji mzima na mabango yao na kuhakikisha kiu yao imekwisha basi waliamua kurudi chuoni

Gari la washa washa nalo lilikuwepo lakini watu walikuwa na jaziba zao vilevile mwanzo mwisho

Barabara zilikuwa zimetawaliwa na wanafunzi kwa kiasi kikubwa, mpaka kusababisha magari kutopita



Hapa ndipo safari ya maandamano ilipoanzia na ndipo safari hiyo ilipoishia maeneo haya ya kwenye bendera mbele ya jengo la administration.

Safari ya maandamano ya amani ikawa imeishia chuoni hapo baada ya kuona kuwa ujumbe wao umefika. Wanafunzi wa chuo wamechoshwa na matendo mabaya ambayo wanafanyiwa ikiwa ni pamoja na kubakwa, kulawitiwa, kuibiwa vitu vyao kama Laptop na vitu vingine. Wameonesha umoja wao kwa sababu ya kuchoshwa na mambo hayo, ambapo jana asubuhi kuna wanafunzi walivamiwa na kuibiwa Laptop. Hivyo wakaamua kujikusanya asubuhi hiyo hiyo mida ya saa kumi na mbili alfajili na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja ambaye walimpiga na baadae kuchukuliwa na polisi.