kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Sunday, June 1, 2014

CHUO CHA MIPANGO DODOMA CHAIBUKA WASHINDI WA FAINAILI YA MPIRA WA KIKAPU ILIYOANDALIWA NA MH ANTONY MAVUNDE MJINI DODOMA,MWENYEKITI WA ASASI YA VIJANA YA "YES" AMPONGEZA ,

Fainali ya mashindano ya mpira wa kikapu yaliyoandaliwa na Mh Anton Mavunde yaliyofanyika weekend hii katika uwanja wa vijana mjini Dodoma na kufikia tamati siku ya jana 31/05/2014 ambapo vijana wa chuo cha Mipango waliibuka kidedea huku wakiondoka vifua juu baada ya kutwaa kombe la ushindi,

Mashindano hayo yalikuwa yakipekee sana yenye maandalizi ya hali ya juu sana ambapo Mgeni rasmi wa mashindano hayo alikuwa ni Mh Juma Nkamia pamoja na viongozi mbalimbali wa nchi na pia kulikuwa na werembo wa Miss Vyuo Vikuu vyote vya tanzania ambao walikuja kumuunga mkono kijana mwenzao Mh Antony Mavunde kwa kuandaa mashindano hayo,Huku warembo hao wakionyesha mbwembwe kidogo huku mashibiki wakifurahia kwa nderemo na vifijo kwa kupata burudani tofauti . Pia baadhi ya vijana walionekana kufurahishwa na mashindano hayo na kumpongeza sana Mh Anton Mavunde kwa kuwajali vijana na kuwakumbuka na kuwasaidia katika namna moja ama nyingine, HONGERA SANA MH ANTON MAVUNDE

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Youth Empowerment and Support (YES)  Bw. Remidius Emmanuel amempongeza  Bwana antony mavunde kwa kuwa mstari wa mbele   kujumuika katika shughuli mbalimbali za vijana hususani michezo.



































No comments :

Post a Comment