kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Monday, August 19, 2013

SIMANZI: MWANAFUNZI MWINGINE WA CHUO CHA CBE AFARIKI DUNIA.

  MAREHEMU  SHIJA  MANYALILA


Ikiwa ni wiki chache tangu Chuo hiki cha Elimu ya Biashara Kampasi ya Dodoma  kiondokewe na Mwanafunzi ( Marehemu Restuta Mayuma  mnamo Tarehe 05/08/2013) Chuo hiki kwa mara nyingine kimepata pigo kwa siku ya  jana (Tarehe 18/08/2013 siku ya Jumapili)  Mnamo saa 12 Asubuhi Baada ya Mwanafunzi wa Chuo Hicho  Ndugu  Shija  Manyalila Kufariki dunia baada ya kusumbuliwa  na Homa  pamoja na Malaria.
Akizungumza na Blogu yetu  Ndugu wa Marehemu Bw.Paschal  Amesema Marehemu  wiki chache zilizopita Alikuja Dodoma (Chuoni) kufanya Mitihani yake ya Supplimentary/Special  na kisha  kurudi makwao  Mkoani Shinyanga Eneo la Kolandoto  KM 40 kutoka Shinyanga Mjini kama unaelekea Mkoani Mwanza.Ambako hali yake ilibadilika mpaka kupelekea kifo chake.
Kwa mujibu  wa Bw. Paschal  amesema Mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatano  Tarehe  20/08/2013 Mkoani Shinyanga.

Mwanafunzi huyo aliyekuwa anasoma  Diploma ya Uhasibu  Mwaka wa kwanza  mkondo "C" kwa mwaka wa masomo 2012/2013, Ameibua simanzi miongoni Mwa wanafunzi wa Chuo hicho.

Blogu hii ilipojaribu kuzungumza na Mshauri wa Wanafunzi wa Chuo cha CBE Kampasi ya Dodoma Amekiri kupata taarifa hizo na kwamba bado chuo kinaendelea kufanya taratibu zake kwa nafasi yake.

"TUNAWAOMBEA KWA  MUNGU NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI WA  MAREHEMU  SHIJA  , MUNGU AWATIE NGUVU KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU"

AMINA.

Tuesday, August 6, 2013

MWANAFUNZI WA CBE KAMPASI YA DODOMA AFARIKI DUNIA (05/08/2013)


 
MAREHEMU    RESTUTA  MAYUMA

Ni masikitiko makubwa kwa wanafunzi wa Chuo Cha Elimu ya Biashara (CBE)  kampasi ya Dodoma  kwa kumpoteza mwanafunzi mwenzao  Bi. Restuta Mayuma ambaye alifariki tarehe  05/08/2013 (Jumatatu) mnamo mishale ya saa kumi na moja jioni.
 Hata hivyo mwanafunzi huyo  alikuja dodoma kwa lengo la kufaya mitihani yake ( katika kipindi hiki ambacho wanafunzi wa Chuo cha CBE  wamekuwa wakiendelea kufanya mitihani yao ya Special pamoja na ile ya Supplimentary.
Marehemu Restuta, Alikuwa anasoma Diploma , kozi ya Uhasibu (Accountancy) , ambapo alianza masomo ya Diploma mwaka wa masomo 2011/2012 na alitakiwa kuhitimu  Elimu yake  ya Diploma  mwaka 2012/213.Lakini  kwa kipindi hiki alikuja  chuo kurudia mitihani yake ya Diploma  I  .
Akizungumza  na Univesities Corner  Rafiki wa karibu sana na Mwanafunzi huyo (Marehemu Restuta)  alisema  Marehemu alikuwa anasumbuliwa na homa za hapa na pale (Malaria)  hali ambayo ilipelekea  mpaka kutokea kwa kifo chake.
 Tayari Mwili wake umesafirishwa leo kuelekea  Mkoani Dar es salaam eneo la BUNJU  kwa ajili ya shughuli za Mazishi ambapo  mwili huo umesafirishwa na Gari la Chuo (CBE)  Kwa kuambatana na  WARDEN, Mashauri Machunde (Mwanafunzi CBE)  pamoja na baadhi ya ndugu wa marehemu waliokuwepo mkoani Dodoma.

 Akizungumza kwa njia ya simu, Bw. Mashauri Machunde  (Mwanafunzi  CBE)  amewataka wanafunzi wote wa CBE wanaoishi jijini Dar es salaam kijitokeza katika mazishi ya  Mwanafunzi huyo   yanayotarajiwa kufanyika   kesho  nyumbani kwao "Bunju " Kwa kupanda magari yaendayo Bunju na kushukia eneo la Bunju "A" kituo  kinaitwa Shule au Hospital (Uliza kwa Mzee  Mayuma  karibu na Shule ya Sekondari Fanaka)
 Mwili wa Marehemu unatarajiiwa  kuagwa   mnamo saa 7 mchana (07/08/2013)  kabla ya shughuli za  Mazishi kuendelea.
  "Hii ni safari ya kila mmoja , Mwenzetu katangulia . Kwa masikitiko makubwa  Mmiliki wa Blog hii  Bw.Remidius Emmanuel  anatoa pole kwa Familia na ndugu jamaa na Marafiki waliofikwa na Msiba huo"

NOTE: 
Kwa wote walioko Dar es salaam  waweza kuwasiliana na Mashauri Machunde kwa namba : 0652-559011   ili kufika eneo  la msiba (BUNJU)


BAADHI YA PICHA ZA MAREHEMU  (RESTUTA  MAYUMA)  ENZI ZA UHAI WAKE