kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Sunday, May 5, 2013

MWANAFUNZI WA CBE DODOMA APATA AJALI, NI BAADA YA KUGONGWA NA GARI AINA YA NOAH).....

BW. ALFA SANGA    AKIENDELEA KUPATA MATIBABU KATIKA KITUO CHA AFYA  AMANI (AREA  D)
 
Tarehe  03/05/2013  ( Ijumaa)  mnamo mishale ya saa 2  usiku, haitosaulika  Maishani mwa  Mwanafunzi  huyu  Alfa  Sanga  anaesoma   Cheti , course  ya Manunuzi na Ugavi  mkondo C (BCPS  "C") Katika chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi Ya Dodoma.
Akizungumza kwa kirefu,Bw. Emily  Mwandambo (Rafiki wa karibu wa Bw.alfa)  alisema ,   Ajali hiyo ilitokea  Maeneo ya Kibaoni  Area "E"   wakati Bw. Alfa  akiwa na wenzake  wakielekea chuoni  baada ya kufanya discussion na wenzake wanaoishi  Maeneo ya Flamingo.Hata hivyo  wakati  Bw. Alfa akivuka  barabara  (kibaoni -uwanja wa ndege)  Mara ilitokea  gari  aina ya Noah  ambayo ilimgonga  na kupelekea kuumia sana maeneo Kichwani  ambapo alichanika  kiasi flani kisha kuumia zaidi maeneo ya begani. Pamoja na hali hiyo dereva wa gari hilo hakusimama baada ya kubaini  kosa alilofanya.
 Hata hivyo  Mgonjwa huyo anaendelea kupata matibabu katika kituo cha Afya  AMANI  (AREA  " D")  Mpaka jana (04/05/2013  mishale ya saa 11 jioni ) Bw. Alfa alikuwa bado hajapata fahamu.
Universities Corner  inamuombea kwa Mungu  ili apate  kupona na kuendelea na masomo yake.    


     BW. REMIDIUS  EMMANUEL (KULIA)   AKIMJULIA HALI BW. ALFA   SANGA
  BAADHI YA  WANAFUNZI WA CBE   WAKIWA  KITUONI HAPO KWA AJILI YA KUMJULIA HALI MWANAFUNZI MWENZAO.

         MIONGONI MWA MARAFIKI WA KARIBU WA  BW. ALFA   SANGA
        UFAFANUZI UKITOLEWA  NA  NESI WA ZAMU, AKIFAFANUA  JAMBO JUU YA HALI YA MGONJWA.....

Thursday, May 2, 2013

KUMBE FEDHA YA MKOPO NI MOJA YA SABABU YA MWANAFUNZI WA CHUO CHA TUMAINI KUJINYONGA!!!!!

Chuo Cha Tumaini tawi la Dar es Salaam kimepata msiba wa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza aliekuwa anasoma sheria. Mwanafunzi Willhem Mushi mkazi wa Moshi alipoteza maisha baada ya kujinyonga mpaka kufa alipojifungia chumbani kwakeTarehe 29/04/2013 mida ya saa tano asubuhi. Mwili wa marehemu uligundulika kuwa umekufa majira ya saa kumi alasiri chumbani kwake. Mtoa taarifa ambae pia ni mwanafunzi mwenzake ametueleza kwa njia ya simu.

Nini chanzo?!
Kuna taarifa za baadhi ya watu kuwa marehemu Willhem alifikia uamuzi wa kujinyongaa mpaka kufa baada ya kutambua kuwa amefeli (disqualified) masomo yake ya chuo. Sababu hii wengi bado wanaitilia mashaka.
Sababu nyingine ambayo imepata umaarufu zaidi ni ya kwamba marehemu alikuwa akipata pesa kutoka bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu yaani HESLB (wengi huliita BOOM) lakini hakuwaeleza wazazi wake kuwa anapata pesa hizo. Kitendo hicho kilipelekea wazazi wa mwanafunzi huyu kuwa anatumiwa pesa za matumizi na Ada kutoka kwa wazazi wake ili aweze kuendesha maisha yake na kupata elimu ili iweze kumsaidi hapo mbeleni.
Marehemu anadaiwa kuwa alidanganya chuoni kwa mwalimu wake kuwa amefiwa na dada yake kwahiyo hakuweza kufanya test za chuoni hapo kitendo ambacho kilimlazimu mwalimu wake kumpa SPECIAL TEST.
Mzazi wa marehemu Willhem (Baba yake) aliamua kuja kumtembelea mwanae hapo chuoni na kujua maendelea yake hapo ndipo mambo yalipooanza kuharibika kwa ndugu yetu Willhem. Baba alipofika chuoni aligundua kuwa mwanae bado anadaiwa ada na pia amekuwa akipata pesa za mkopo. Mzazi yule pia alishangazwa na maendeleo mabaya ya mwanae hapo chuoni kitaalumu lakini kubwa zaidi ni kupata taarifa ya kuwa WILLHEM HAKUFANYA TEST KWAKUWA ALIFIWA NA DADA YAKE.

Dalili za kifo chake?
Inasemekana kuwa marehemu Willhem kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja alikuwa akilalamika kuwa maisha ni magumu sana kwake na kuwa haoni sababu za kuendelea kuishi. Haya maneno amekuwa akiyazungumza ambapo wanafunzi wenzake wamekuwa wakishangazwa sana lakini hawakujua mwisho wake itakuwa kwa Willhem kupoteza maisha kwa kujinyonga. Willhem alikuwa akiishi maeneo ya Kurasini hapa jijini Dar es Salaam na wenzake watatu. Polisi wanaendelea na uchunguzi kupata taarifa zaidi juu ya kifo cha mwenzetu.