kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Saturday, April 19, 2014

TUYAKEMEE MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA KWA VIJANA

Dar es Salaam. Utumiaji wa dawa za kulevya umekuwa tatizo kubwa linaloikumba dunia hasa wakati huu wa utandawazi, huku sehemu ya waathirika wakuu wa dawa hizo wakiwa vijana ambao ni nguvukazi ya taifa.
Vijana wengi wanaotumia dawa za kulevya wamekuwa wakieleza chanzo kikuu cha wao kujiingiza katika matumizi hayo ni kushawishiwa na marafiki zao na ugumu wa maisha.
Hapa nchini vita ya dawa za kulevya imekuwa kubwa kadri siku zinavyozidi kusonga mbele huku wahusika wakuu wakielezwa kuwa ni vijana. Kundi hili ambalo ni nguvukazi ya taifa, wamekuwa wakitumika kusafirisha sehemu mbalimbali za dunia na nyakati zingine wao wenyewe wakitumia.