Dar es Salaam. Utumiaji wa dawa za kulevya umekuwa tatizo kubwa
linaloikumba dunia hasa wakati huu wa utandawazi, huku sehemu ya
waathirika wakuu wa dawa hizo wakiwa vijana ambao ni nguvukazi ya taifa.
Vijana wengi wanaotumia dawa za kulevya wamekuwa
wakieleza chanzo kikuu cha wao kujiingiza katika matumizi hayo ni
kushawishiwa na marafiki zao na ugumu wa maisha.
Hapa nchini vita ya dawa za kulevya imekuwa kubwa
kadri siku zinavyozidi kusonga mbele huku wahusika wakuu wakielezwa kuwa
ni vijana. Kundi hili ambalo ni nguvukazi ya taifa, wamekuwa
wakitumika kusafirisha sehemu mbalimbali za dunia na nyakati zingine wao
wenyewe wakitumia.
