Naibu Waziri Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh Juma
Nkamia akizungumza na wachezaji kabla ya mchezo huo kuanza.
Fainali za Mavunde Basketball Tournament 2014 zimefanyika leo na kuhudhuriwa na Naibu Waziri Mh Juma Nkamia (Mgeni rasmi), Mbunge wa Sumbawanga Mjini Mh Aeshi, Mhe: Steven Masangia (Diwani wa kata ya Mnadani na Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Ebenezer Destefanos),Washiriki wa Miss Vyuo vikuu, Viongozi wa UVCCM Mkoa na Wilaya ya Dodoma. Fainali hizo zimefanyika leo katika uwanja wa Vijana Youth Centre (Area C) Mjini Dodoma.

