kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Tuesday, April 30, 2013

SIKU CHACHE BAADA YA UCHAGUZI WA CBE- DOM KUTIWA DOA, MIRAJI SIMBA ANENA....

                   BW.   MIRAJI   SIMBA  - MAKAMU WA RAIS  KWA MGOMBEA  MAXIMILIAN  ( CBE DODOMA 2013/2014)

Akizungumza na chanzo chetu cha habari Moja kati ya Wagombea wa kinyang'anyiro cha  Urais CBE-Dodoma Bw. Miraji Simba ambaye ni mgombea Mwenza (makamu wa Rais)  wa MaXimiliani ,Ameibuka na  kuitaka jamii ya wana CBE  kuondoa tofauti mbalimbali na kudumu kama  ndugu jamaa na Marafiki hasa katika nyanja za kitaaluma.
Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku chache tangu vuguvugu la uchaguzi kupungua kasi    hasa baada ya Moja ya Wagombea wa nafasi ya Urais Bw. Dotto Kazi Leonard  kuishitaki Maha
kamani tume  pamoja na Bodi ya Chuo kwa  kwa madai ya kutotendewa haki  juu ya kuondolewa kwake katika kinyang'anyiro hicho.
Katika hatua nyingine Bado Bw. Remidius Emmanuel Ameendelea kung'ara na kukubalika kama mkombozi mkuu wa jamii ya wana CBE  kufuatia uwezo na historia aliyonayo  katika nyadhifa alizo wahi kuongoza katika vyuo mbalimbali hapa Tanzania.
Maamuzi ya Mahakama yamekuwa yakisubiliwa kwa hamu kubwa  ingawa kumekuwepo na hali ya wasiwasi kwa wanafunzi walio wengi kwa kuamini kuwa huenda uchaguzi usifanyike tena. Akizungumza  kwa Masharti ya kutotaja jina Mwanafunzi mmoja amesema  wao kama wanafunzi wanayo haki ya kuwa na uongozi   kupitia njia ya kidemokrasia  na hivyo wanaamini Professor  Mjema  atalisimamia suala hilo.