kuza biashara yako

kuza biashara yako

Pages

Monday, December 31, 2012

MAZISHI YA MWANAFUNZI WA UDAKTARI ALIYEBAKWA YAFANYIKA..









Maombolezo nchini India
 
Hatimaye mazishi ya mwanafunzi wa Udaktari aliyefariki juzi jumamosi katika hospitali ya Mount Elizabeth nchini Singapore yamefanyika huko India. Juhudi za Madaktari kuokoa maisha yake zilishindikana kutokana na kuathiriwa zaidi na unyama aliofanyiwa na kundi la wanaume sita katikati ya mwezi huu.

Mwili wa mwanamke huyo aliyekuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu tayari uliwasili nyumbani mapema jana asubuhi na kupokelewa kwa heshima kubwa ambapo Waziri Mkuu wa India Manmohan Singh naye alikuwepo katika mapokezi hayo.

Maelfu ya raia nchini India juzi jumamosi waliendelea kukusanyika katika mji mkuu New Delhi wakiwa na mishumaa kama ishara ya maombolezo ya kifo cha mwanafunzi huyo aliyebakwa ndani ya basi katikati ya mwezi huu.

Kwa takribani majuma mawili kumekuwa na ghasia kubwa nchini humo waandamanaji wakipinga unyanyasaji dhidi ya wanawake na kutaka adhabu ya kifo itekelezwe kwa wanaotuhumiwa kwa tukio hilo.

Wanaume sita wanaoshikiliwa kwa kufanya unyama huo sasa wanakabiliwa na kesi ya mauaji ya binti huyo aliyefariki juzi asubuhi katika hospitali ya Mount Elizabeth nchini Singapore ambako alipelekwa kwa matibabu zaidi.

Saturday, December 29, 2012

HALI HII INALETA MATUMAINI KWA WANAVYUO MKOANI DODOMA


           Muonekano wa   Sasa  wa  Eneo la Jamatini  kituo cha daladala  kinachofanyiwa  ukarabati na maboresho ya hali ya juu.

Hatua hii imeonekana kuleta matumaini makubwa Miongoni mwa wanachuo wengi kutoka vyuo mbalimbali   mkoani hapa.
Mara nyingi  wanafunzi wengi wa Elimu ya juu  wamekuwa ni miongoni mwa  watu wanao kubwa  na  tatizo la  usafiri  kuelekea  vyuoni, hata hivyo matatizo hayo yamekuwa yakisababishwa na   na sababu nyingi  ikiwemo miundo mbinu ambayo kwa kiasi kikubwa  imekuwa ikichangia  uwepo wa changamoto hizo.
Baadhi ya wamiliki wa Daladala  wakizungumza na Dodoma universities corner  wamesema  ' ni kweli wakati mwingine wanashindwa kuleta  magari yenye ubora  kufuatia hali ya miundo mbinu na hivyo kutoa kipaumbele kwa magari ambayo  tayari yamefanya kazi mikoa mingine, hivyo hatua ya Serikali kutengeneza  na kuboresha Kituo cha jamatini na sehemu nyingine za manispaa  mkoani hapa kita chochea uwekezaji mkubwa  katika nyanja hiyo. 

 Muonekano wa kituo cha Daladala  kinachotumika sasa , Ambapo hatua ya kukamilika kwa ujenzi wa kituo cha Jamatini  kutaondoa misongamano  na kuleta mpangilio mzuri wa  Huduma ya  Usafiri katika manispaa ya Dodoma mjini

MWANACHUO AZIDIWA AKIWA DARASANI, NI BAADA YA KUUGUA GHAFLA...

  
 Mwema  Machage   akiendelea kupata huduma baada ya kutundikiwa Drip

 
 Mwanafunzi wa chuo cha ST. JOHN   mkoani Dodoma  Juzi jioni (Alhamisi)  alizidiwa Ghafla akiwa darasani baada ya  kuishiwa nguvu ghafla. 
Mwanafunzi huyo aliyefahamika kwa jina  la Mwema  E. Machage   anayesoma  Bachelor Degree in  Business Administration Mwaka wa kwanza  akizungumza na  Dodoma Universities Corner   alisema   yeye  alikuwa  darasani  kisha  akajisikia mwili  unaisha nguvu   hatua iliyo  lazimu kupelekwa Kituo cha Afya  cha AMANI (AMANI Health Centre) Ambako alilazwa  baada ya kubainika  kuwa alikuwa akisumbuliwa na malaria.
Hata hivyo  Mwana chuo Huyo mpaka leo hii (jumamosi) bado  Amelazwa Hospitalini  hapo  akiendelea kupata matibabu.Ingawa hali ikiendelea vizuri huenda akaruhusiwa leo.
Baadhi ya wanachuo wakiwasili katika kituo  cha Afya  AMANI  kwa ajili ya kumjulia hali  Mwanachuo huyo (MWEMA)

    Bw. Boaz   Elius  Mwanachuo wa  UDOM  Akimhudumia  Mwema  baada ya kumtebelea  Kituoni hapo.



Tuesday, December 25, 2012

SIKU KUU YA X-MASS- UDOM KAMA MBAGALA, NAULI EDUCATION (NG'ONG'ONA) YAPANDA NA KUFIKIA 1500/=

 kufuatia siku kuu ya Christimas Hali  ya sintofahamu imeibuka leo  katika standi ya Mabasi madogo  ( Daladala)  kwa magari yaendayo chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) baada ya  ongezeko la Abiria (wanachuo) kuwa wengi  ikilinganishwa   na magari yaliyokuwepo.
Kufuatia hali hii  wanachuo wengi hususani kitivo cha  Elimu (Education) wamejikuta katika wakati mgumu sana  na wengine kulazimika  kupanda magari  aina ya Noah  kwa garama ya shilingi 1500. 

          Baadhi ya  Wanachuo wakionekana  kukata tamaa...
                             Wengine wakalazimika kucheka.....

                Hawa  wakishuka kutoka UDOM...
     Baadhi yao  Wakitafakari hatima ya kupata usafiri kurudi chuoni. 
                                           Usafiri  hakuna kabisa....

                              Kweli hii ni kama mbagala...



         Baadhi ya wanachuo wakipambana ili kuingia ndani ya gari






        Baadhi ya  Wanachuo wanaamua kupanda Magari aina ya Noah...




   Dereva  wa moja kati Gari hizo (Noah)  akichukua  Nauli yake kwanza..
      Muonekano  wa sehemu ya barabara  katika standi hiyo ya Daladala


Monday, December 24, 2012

KUELEKEA SIKU KUU ZA CHRISTMAS NA MWAKA MPYA, WENGI WANENA...

  Naitwa  Luhaga J. Mpina  Kamishina wa TCU ,Mbunge wa jimbo la Kisesa  na Mbunge wa Bunge la  Afrika  Nawatakia  Wanachuo wote wa vyuo vyote vya Tanzania   Heri ya sikukuu za  Kristmas na Mwaka mpya.
 
Naitwa Egubo Jason  Spika wa Bunge la Wanachuo ,Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE)  Kampasi ya Dodoma . Nawatakia  Wanachuo wote wa Mkoa wa Dodoma  Heri ya sikukuu za  Kristmas na Mwaka mpya.Kwa upekee mkubwa  Nawakumbuka pia Waheshimiwa wabunge wote wa Bunge la wanachuo CBE .  

Kutoka Chuo kikuu cha St.John, Tunawatakia  Wanachuo wote wa Mkoa wa Dodoma  Heri ya sikukuu za  Kristmas na Mwaka mpya.
Naitwa Boaz  Mwema  Mwanachuo ,Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM),Nawatakia heri ya christimas na Mwaka mpya  wanafunzi wenzangu  wanaosoma Sheria mwaka wanne UDOM.
Lakini kwa upekee mkubwa  naikumbuka familia yangu  pamoja na Mama yangu mzazi bila kumsahau Baba yangu mzazi Mzee Elius  Mwema.

Naitwa Ester Lukas Mfanyakazi wa Chuo cha Elimu ya Biashara CBE- Dodoma  nawatakia Nawatakia sikukuu njema    wote wanaonifahamu 

Naitwa  Baraka Emmanuel (King Barry Joe)  Mwanachuo chuo Cha Mipango,Ni jambo la kumshukuru Mungu na kumtanguliza mbele katika kila jambo tulitendalo katika msimu huu wa sikukuu, yatupasa kukaa chini na kutafakari juu ya mambo tulio yafanya ndani ya mwaka huu mzima, je, ni malengo mangapi tulio jiwekea na kuyatimiza? na ni malengo mangapi hayakutimia na i kwasababu gani? ili kufanikisha  malengo yetu kwa mwaka ujao.

Nawatakia Sikukuu njema wanachuo wote MIPANGO, CBE, UDOM, ST. JOHN na HOMBOLO iwe ni siku yenye mafaniio makubwa kwenu na mwanzo wa mafanikio na mipango mingine ya maendeleo.

Pia napenda kuwatakia siukuu njema Wazazi wangu na ndugu zangu wote pamoja na  wanachuo wenzangu wote wa MIPANGO bila kuwashau marafiki zangu wa karibu Adam Kitembe, Joseph, Yassin, Actar, Good omy giver na wengine wote.

Mwisho kabisa namuomba Mwenyezi Mungu atuongoze tusherehekee salama siukuu hizii na atuongoze kwa kila jambo.

*******MARRY CHRISTMAS AND HAPPY NEW YEAR**********


 hi ,Naitwa  Mammy Swai nawatakia heri ya chxmas +mwaka mpya marafki zangu wote wanaonifahamu bila kuwasahau wazazi wangu popote walipo nawapenda sana,this wishes ziende to all my clasmet,teachers etc.NAWAPENDA WOTE
Naitwa  Juvenal Gasper ,Salamu zangu ziende kwa familia ya mr and mrs boaz mwema  na wahitimu wote wa chuo kikuu cha dodoma 2011_2012 ujumbe katika kipindi hiki cha sikuku tusherekehe x mass kwa amani na upendo
Naitwa Remidius  Emmanuel, Mkurugenzi  mtendaji wa  Blog ya Dodoma Universities Corner.Nawatakia heri ya Christimas na Mwaka mpya wanachuo wote  wa mkoa wa Dodoma.


Naitwa Dickson Kanje, Safari ya miezi 12 ya mwaka 2012 imefikia ukingoni wapo tuliokwaruzana kwa sababu mbali mbali wapo tuliosaidiana kwa uwezo wa Mungu na juhudi za pamoja nawataka radhi wale wote niliowakwaza na nawapongeza wale wote tuliosaidiana tuendelee kushikana zaidi kwa mwaka unaokuja tukiwa tumesamehe yote ya mwaka huu kwa waliotukwaza merry christmass happy new year.



 Boss ngasa.blogspot.com pamoja na G&G internet Cafe Dodoma inakutakia heri na mafanikio katika sikukuu ya xmass na mwaka mpya

Naitwa  Saida Amour  Mwanachuo Chuo Cha elimu ya Biashara  CBE -DOM Nawatakia  Wanachuo wote wa Mkoa wa Dodoma  Heri ya sikukuu za  X-mas na Mwaka mpya
Naitwa  Bahati Njakachai  Kwa sasa niko Dar es salaam , Nawatakia  Wanachuo wote wa   CBE   Heri ya sikukuu za  X-mas na Mwaka mpya


 Robert Mkuchu senior famous wishing you merry x mass and happy new year
Naitwa Abel Laiser  Nawatakia Heri ya Christmas na Mwaka Mpya  Watu wote wanao nifahamu.

Sunday, December 23, 2012

HII NI FUNGA MWAKA , NI KATIKA CHUO CHA UDOM BLOCK ' M ' a.k.a MILLENIUM TOUR

Wanachuo hao waamua kujipa raha wenyewe baada ya ukimya sana chuoni hapo na kuamua kuchangamsha Hostel kwa kufanya Party. ambapo Block M ndiyo Block  ambayo mara nyingi imekuwa ikileta  hamasa mbalimbali za burudani na kuwa na uchangamfu wa kipekee. Hata hivyo baadhi ya Wanachuo  walionekana  kufurahishwa na hatua hiyo huku wengine wakisema  sio wakati wote   ni kusoma badala yake  akili zetu zinahitaji kuburudika  na kupata vitu  vipya  kwa lengo la   kuzifanya  bongo zetu kurudi katika  hali ya kawaida na wakati mwingine kupunguza stress mbalimbali za kimaisha.  

baadhi ya wanachuo wa Udom wakimwangalia mwenzao akicheza mziki nje ya hosteli zao.

Saturday, December 22, 2012

HUYU NDIYE MWANACHUO WA CBE -DODOMA ALIYE FANYA MAAJABU...


                                                   MR.Leonard  L. Sylvester

  MR.Leonard  L. Sylvester, Ni mwanachuo wa chuo cha Elimu ya Biashara (CBE)  Kampasi ya Dodoma  ambaye amethubutu kutunga kitabu  chenye jina la " WAWEZA KUWA VILE UTAKAVYO"  hatua inayomfanya  kuanza kutimiza ndoto zake  katika hatua za awali.Bw. Leonard  anaonekana kijana mwenye kujiamini na kwamba  hapa duniani kila kitu kinawezekana kama ukitia nia ya dhati kwa kuwa na malengo  ya kile utarajiacho kufanya.  Universities Corner ilikutana na  Mwanachuo huyu na kutaka kujua  jinsi alivyo weza kuanza  au kupata wazo hili. Leonard anasema:-

  WAWEZA KUWA VILE UTAKAVYO  Ni kitabu nilichoandika kinachohusu kujitambua kwa mtu kuwa anaweza kuwa vile atakavyo katika maisha yake pasipo kuangalia amezaliwa katika mazingira yapi au anapitia mazingira yapi.
Ndani ya kitabu hiki utapata kufahamu mambo mengi ambayo yanagusa maisha ya mtu binafsi, katika maisha yake, changamoto anazokabiriana nazo na njia au mbinu za kuzikabiri changamoto na kufikia pale alipo azimia kufika kwa msaada wa Mungu.
·         Ndani ya kitabu hiki utapata kufahamu kuwa ndani yako unao uwezo wa kuumba au kufanya jambo lolote hapa duniani.
·         Utapata kufahamu vizuizi unavyopata katika kuyaendea mafanikio yako.
·         Umuhimu wa kuyaombea mafanikio yako.
                    
                                    Muonekano  wa   cover  la  kitabu hicho


          
         HISTORIA FUPI YA KATIKA KUKIANDIKA HIKI KITABU
Kwanza natanguliza shukrani zangu kwa Mungu kuniwezesha na kunifanikisha mpaka kukiandika hiki kitabu na kikawa msaada mkubwa kwa jamii.
Siku ya kwanza nilipopata wazo la kuandika kitabu nilikuwa nimemaliza form four mwaka 2006 kipindi hicho nilikuwa nina shahuku nifanye jambo gani ambalo litakuwa msaada kwa jamii inayonizunguka. Siku moja nilikuwa kwenye semina ya Neno la Mungu Kanisani ninaposali, Mtumishi mmoja wa kimataifa aitwaye DR. TAYO  kutoka Uingereza alikuwa akifundisha kuhusu kufanya jambo la kipekee ambalo jamii itafaidika na hata ukifa utakumbukwa kwa hilo jambo ulilofanya.
Hapo ndio nikapata wazo la kuandika kitabu. Binafsi napenda kufanikiwa na kuwa mtu wa tofauti kila mahali niendapo. Ndipo nikapata wazo la kuandika kuhusu mafanikio. Nilianza kuandika hiki kitabu mwaka 2009, nilitumia miaka mitatu kukiandika hiki kitabu hadi mwaka huu 2012 ndo nilikikamilisha.
Haikuwa rahisi kuandika kitabu kama unavyofikiria, ni kwa neema ya Mungu tu. Maana changamoto ni nyingi,

         BAADHI YA CHANGAMOTO NILIZOPOTIA.  
1.    Niliandika mpaka karatasi 17 Laptop iliharibika na data zote zikapotea ikabidi nianze upya, sikukata tamaa, maana nilidhamiria toka moyoni kuandika kitabu.
2.    Kukatishwa tamaa na watu kuwa hauwezi kuandika kitabu kwa sababu mimi ni kijana mdogo.
3.    Pia na wengine walisema kitabu hakitawafikia wengi kwa sababu sijulikani kwa watu.
Lakini mimi sikuangalia waliyosema bali niliangalia moyoni mwangu nimedhamiria kuandika kitabu ili jamii ipate kujua maarifa niliyonayo katika Yesu Kristo kwa habari ya mafanikio ya mtu na kujitambua kwa mtu kuwa anaweza kuwa vile atakavyo katika maisha yake.
Maana nilijitambua kuwa NAWEZA KUWA VILE NITAKAVYO na siyo mtu mwingine atakavyo.
Namshukuru Mungu alinipigania mpaka nikafika hatua ya kuki-publish na mpaka sasa kitabu kinapatikana Bookshops, na watu washavipata.
Pia namshukuru Mungu napigiwa simu na watu wakimtukuza Mungu kwa kuguswa katika maishha yao kupitia kukisoma hiki kitabu pia nimeshaitwa kuendesha semina Dar es Salaam kuhusu hiki kitabu kwenda kufundisha vijana.
Watu wengi wamebadilishwa maisha yao, fikra zao, mitazamo yao baada ya kukisoma hiki kitabu.
Kwa hiyo ni jambo la kumtukuza Mungu kufikia hatua hii maana nilijitambua kuwa naweza kufanya jambo lolote nikiamua.
         USHAURI WANGU KWA VIJANA WOTE, WANACHUO.
Jambo la muhimu sana la kufanya kwanza ni KUJITAMBUA. Jitambue kuwa wewe ni mtu wa tofauti sana na ni wakipekee kuliko mtu mwingine yeyote maana kama Mungu angetuumba wote sawa, basi kulikuwa hakuna haja ya wewe kuwepo duniani.
Mungu amekuleta hapa duniani akakufanya wa tofauti, ili uweze kufanya mambo ya tofauti katika jamii ili jamii ikawe ya tofauti.
 (Ngoja nikupe mfano wa kibiologia ili uone kuwa wewe wa pekee)
Utaona aibu ila ndiyo ukweli wenyewe; weka maanani.
Mwanaume anazalisha mbegu za kiume milioni kwa siku  na siku mimba yako inatungwa zilikuwa mbegu nyingi zilitoka lakini mbegu ya kiume moja tu ikawahi kuingia kwenye yai la mwanamke, ndo wewe ukazaliwa, na kumbuka mbegu nyingine pia wale walikuwa watu lakini Mungu akaona wewe ndo uje duniani, je hile mbegu ya kiume ambayo ni wewe isingewahi kwenye yai je ungukuwepo leo? (Hebu jiulize hilo swali).
Hapo ndiyo utakapojua kuna umuhimu wa wewe kuwepo hapa duniani kwa ajili ya kusudi maalum.pia hupo hapa chuo kwa kusudi maalum hausomi kwa sababu wazazi wamekuleta kusoma bali lipo kusudi la wewe kuwa hapa chuo kusoma.
Vijana wenzangu, haijalishi unaishi mazingira ya namna gani tambua kuwa unaweza kufanya jambo lolote katika maisha yako kama ukiamua. Usijidharau kama una wazo la kuandika kitabu anza taratibu, kitabu hakiandikwi siku moja, anza taratibu, kama wewe unataka kufanya biashara wakati unasoma anza hakuna anayekuzuia (You can do int) amun kufanya jambo
 (STOP DREAMING JUST MAKE IT HAPPEN)
Kuwa na matarajio ambayo unajua utaweza kuyatimiza.
SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA UJANA WAKO
1.   Penda kujitamkia mawazo mema(Think positive) hata kama mazingira magumu na jitamkie kuwa unaweza kuwa vile utakavyo. Katika masomo yako jitamkie kuwa wewe ni mshindi na siyo kushindwa hata kama hauelewi darasani. Siku zote kumbuka kinywa kinaumba na Neno la Mungu linasema AWAZAVYO MTU NAFSINI MWAKE NDIVYO ALIVYO.
Kwa hiyo ulivyo sahivi ni matokeo ya ulikuwa unajiwaziaje kipindi cha nyuma.

2.   Penda kusoma vitabu vya watu waliofanikiwa.
Jenga tabia ya kusoma vitabu. Kuna msemo wanasema (If you want to hide a black people something write it in the book).
Jiulize mpaka sasa umesoma vitabu vingapi ukiachana na vya darasani. Uwe na tabia ya kusoma vitabu ujue mbinu za kufanikiwa na kuwa wa tofauti ili kila mtu akuonapo amtukuze Mungu na awe na shauku ya kuwa watofauti na yeye.
Mimi ninapenda sana kusoma vitabu na ukitaka uhakika uliza marafiki zangu wa karibu watakuambia. Nyumba nakaribia kufungua home library kwenye room yangu kwa vitabu nilivyonavyo vya Kiswahili na kiingereza, napenda kusikiliza mahubiri kwa watu waliofanya mambo makubwa hapa duniani.
Kwa kufanya hivyo nimepata kujitambua na kuwa wa tofauti na yapo mambo makubwa nitaenda kuyafanya mbeleni.
3.   Penda kuwa na marafiki wenye akili
Kuna msemo unasema (Show me your friend and I will fell your who you are). Je marafiki zako ulionao wanakufanya usonge mbele? Au wanakurudisha nyuma? Ebu kuwa na marafiki ambao mkikaa dakika 5 unakuwa ume-gain jambo la kimaisha na siyo kukaa na kupiga porojo.
Mimi watu ninaoshirikiana nao mambo ya ndani sana katika maisha ni watu walionipita umri pia wanajitambua wao ni akina nani. Kwahiyo Napata maarifa kiasi kwamba nikifanyia kazi maarifa niliyopata popote nitakapokwenda ninakuwa wa tofauti.

4.   Penda kuandika malengo yako kwenye Notebook.
Vijana wengi wanapenda kuwish  (I wish to have a good house, I wish to have a good wife, I wish to have a nice job). Siyo vibaya ku-wish swali linakuja how will you do to reach of what your wishing for? Hilo ndo tatizo la vijana wengi. (Stop wish, just make it happen).
Ukiwa na tabia ya kuandika yale unayo-wish ni rahisi kuyafuatilia ni namna gani ufanye ili kuyafikia malengo yako, na pia itakupa wahisi kutaombea malengo yako.

NOTE:
Vijana wenzagu tuache mambo ya kuigaiga hebu amua kuwa mtu halisi, jikubali (Proud yourself) maisha ya kuiga hayapendezi bali kuwa vile Mungu anataka uwe, watu wakikucheka usione aibu ni bora wakakucheka lakini umejitambua ulivyo kuliko kuiga ukaonekana kituko.
Tatizo la Waafrika na Watanzania (WE ARE SUMMARIZE A SUMMARIZED SUMMARY)
Amua kuwa wa tofauti na utaweza kuwa vile utakavyo.
Mungu wangu awabariki sana.
Ukihitaji kitabu wasiliana na mimi.



                                                                            Leonard  L. Sylvester (Facilitator)
                                                                             BBA  I
                                                                             0768 089000
                                                                             leonardsylvester@yahoo.com